Tamko la katibu katika wizara ya ardhi Kombo Mwero kuwa watu wa pwani hawawezi kupata nyadhifa kuu katika afisi za serikali kwa vile hawana elimu limewakasirisha mno wasomi wa mkoa huu ambao sasa wanamtaka katibu huyo aombe msamaha.Katibu Mwero akiongoea katika ukumbi wa mkuu wa mkoa wa pwani wakati wa kongamano la ustawi kufikia mwaka wa 2030,alidai wakazi wa mkoa wa pwani hawajaweza kuajiriwa kazi kubwa kwa kukosa elimu.
Hata hivyo Sheikh mmoja ambaye alisomea sana mambo ya baharini aliinuka na kumkashifu katibu huyo kwa ujeuri huo huku akisema kuwa licha ya yeye kusoma sana,bado hajapata kazi katika shirika kubwa kama vile KPA.
Sasa maoni kwenu watu wa pwani,je? katibu huyu alikuwa na maana gani aliposema watu wa pwani hawakusoma.
Tafadhali leteni mchango wenu katika blog hii ili tuendeleleze hoja hii.
Kazungu Samuel
Hata hivyo Sheikh mmoja ambaye alisomea sana mambo ya baharini aliinuka na kumkashifu katibu huyo kwa ujeuri huo huku akisema kuwa licha ya yeye kusoma sana,bado hajapata kazi katika shirika kubwa kama vile KPA.
Sasa maoni kwenu watu wa pwani,je? katibu huyu alikuwa na maana gani aliposema watu wa pwani hawakusoma.
Tafadhali leteni mchango wenu katika blog hii ili tuendeleleze hoja hii.
Kazungu Samuel
Comments