Mwakere asitingisike awe imara

Namuomba waziri Ali chirau Mwakere asibabaike bali awe imara kwani wabunge wenzake wanamuunga mkono.Ukweli ni kwamba viongozi hawa ambao wanasema kuwa bandari ya Mombasa iongozwe na afisa wa kitaifa badala ya mpwani ndio wale wale ambao walisema wanataka mkoa huu wa pwani ujiendeleze na hata wakatoa ajenda nyingi tu ikiwemo suala la Majimbo.Ni jambo la kushangaza kuwa hawakuwa na utaifa huu ambao sasa unajitokeza.Hii ni changamoto kwa wabunge wa pwani kuwa wafanye juu chini na kuongea kwa sauti moja ili bandari hii ya Mombasa ibaki katika himaya ya pwani.

Comments