MWAMBAO SANAA GROUP KUTOA FILAMU MWEZI HUU


Wasanii wa maigizo kutoka kikundi cha Mwambao Sanaa Group wanatarajiwa kutoa filamu ya kiswahili ambayo inatarajiwa kuwa na ubora wa filamu za kiswahili Afrika Mashariki na Kati.


Filamu hiyo ambayo inajulikana kama DENI ilitungwa na kuelekezwa na mwandishi maarufu wa makala jijini Mombasa Bw.Kazungu Samuel.


Upigaji picha wa filamu hiyo ulifanywa na Justine Katana wa kampuni ya CK Production iliyoko viungani mwa jiji la Mombasa katika mtaa wa Mgongeni-Mwandoni.


Kikundi cha Mwambao Sanaa Group kinapatikana katika eneo la Steji ya Paka huko Bamburi.
Kwenye picha hapo juu,afisa wa uhusiano mwema wa kikundi hicho cha wasanii Bi.Salma Abdalla anaonekana akimpa cheti mwenyekiti wa kikundi hicho Bw.Ludovick Mbogholi pindi tu alipokipata cheti hicho.
Mpiga Picha:Kazungu Samuel

Comments