SHIDA YA MAJI IMEKUWA DONDA SUGU HUKU KILIFI MKOANI PWANI











Unapopita katika maeneo mengi ya mashambani wilayani Kilifi ni kawaida kuwaona akina mama na watoto wakitembea mwendo mrefu kutafuta maji.








Hali hii imezidishwa na kiangazi cha muda mrefu katika eneo hili ambalo linapakana na mbuga ya wanyama ya Tsavo Mashariki.








Nilipofika huko majuzi,nilikumbana na akina mama wakichimba bwawa ili kutega maji wakati mvua itakaponyesha.Lakini hii pia sio kazi rahisi kama picha hizi zinavyoonyesha.Matatizo kweli ni mengi vijijini.








Tunaweza kuwasaidia wakazi hawa kivipi.




Comments